MTOTO WA MIEZI MIWILI ANAJISIWA
Tukio hilo limekuwa gumzo katika mitaa mbalimbali wilayani humo,
huku baadhi ya wananchi wakidai kuwa linahusiana na imani za
kishirikina.
Unaweza kujiuliza maswali mengi, hata inakuwaje mtoto wa miezi miwili kunajisiwa?
Katika vijiwe vya kahawa wilayani Mpwapwa, hii ni habari kubwa zilizokuwa zikizungumzwa kuhusu kunajisiwa kwa mtoto huyo swali likibaki; Je, yule mtu alimnajisi mtoto ameishia wapi?
Katika vijiwe vya kahawa wilayani Mpwapwa, hii ni habari kubwa zilizokuwa zikizungumzwa kuhusu kunajisiwa kwa mtoto huyo swali likibaki; Je, yule mtu alimnajisi mtoto ameishia wapi?
Naingia chumba cha Mganga Mkuu Wilaya ya Mpwapwa
kupata maelezo ya mtoto huyo tangu alipofikishwa katika hospitali ya
wilaya hiyo, maendeleo yaliyofikiwa na utaratibu wa kiuchunguzi
unavyoendelea.
Kauli ya Mganga Mkuu
Mganga Mkuu wa Hospitali ya Wilaya ya Mpwapwa, Lunemo Sakafu anasema kuwa tangu alipolazwa, mtoto huyo alikuwa akipelekwa kliniki kwa ajili ya kupatiwa chanzo mbalimbali na kupima afya yake, kwamba alikuwa na afya nzuri.
Mganga Mkuu wa Hospitali ya Wilaya ya Mpwapwa, Lunemo Sakafu anasema kuwa tangu alipolazwa, mtoto huyo alikuwa akipelekwa kliniki kwa ajili ya kupatiwa chanzo mbalimbali na kupima afya yake, kwamba alikuwa na afya nzuri.
“Hakuzaliwa katika hospitali hii ila alikuwa
akihudhuria kliniki, alizaliwa kwa wakunga wa jadi na mara ya mwisho
kuja hapa hospitali ilikuwa Aprili 15, mwaka huu na alikuwa na afya
nzuri,” alisema
Ashangazwa
Alisema kuwa alishangazwa na hali aliyokuwa nayo mtoto huyo alipofikishwa kwa mara nyingine katika hospitali hiyo kwani alikuwa akitokwa haja zote bila kikomo.
Alisema kuwa alishangazwa na hali aliyokuwa nayo mtoto huyo alipofikishwa kwa mara nyingine katika hospitali hiyo kwani alikuwa akitokwa haja zote bila kikomo.
“Tunampatia matibabu ya kina ili kujua tatizo ni
nini. Kwa sasa tuna utaratibu wa kumpeleka katika Hospitali ya Rufaa ya
Dodoma ili akafanyiwe vipimo vya kina kwa kuwa mtoto huyu anatoa haja
zote bila kikomo,” anasema Sakafu.
Sakafu anasema hata wazazi wa mtoto huyo
walipoulizwa juu ya hali aliyonayo mtoto wao, walipishana kauli katika
maelezo yao na kwamba jambo hilo liliwatia shaka. SOURCE.....MWANANCHI
Post a Comment