MAISHA BASEMENT: Burudani zitakuwa zikianza JUMATATU mpaka JUMATATU, soma zaidi hapa
Maisha Basement zamani ilikuwa ikiitwa NEW MAISHA CLUB kwa sasa
imehamia Makumbusho Kijitonyama jengo jipya la LAPF TOWERS. Club hii ni
mpya na ya kisasa yenye uwezo wa kuchukua watu mia saba (700) yenye
vifaa vya kisasa na dance floor ya kisasa yenye uwezo wa kurusha
matukio live kama video na mechi za mpira.
Uzinduzi wa Maisha Basement utafanyika kwa siku 3 tofauti, uzinduzi wa
kwanza utakuwa Jumatano ya tarehe 15.07.15 ambapo tutazindua na watu
maarufu mbalimbali, na uzinduzi wa pili utakuwa Alhamis ya 16.07.15 na
siku hii tutawaalika watu mbalimbali kutoka katika makampuni (Corporate
People).
Na uzinduzi rasmi wa MAISHA BASEMENT utakuwa siku ya EID MOSI, ambapo
tutakuwa na burudani mbalimbali, na mgeni rasmi atakuwa ni mkuu wa
wilaya ya KINONDONI Mh PAUL MAKONDA. Siku hii kiingilio ni shiling elfu
10 tu. Burudani zetu zilikuwa zinaanza Jumatano mpaka Jumapili, lakini
hapa Maisha Basement burudani zetu zitaanza Jumatatu mpaka Jumatatu.
Post a Comment