Header Ads

Diamond Apost Picha Akiwa Na Wanae, Je.. karudiana Na Zari?


Baada ya tetesi nyingi kusambaa kwamba mwanamuziki Diamond Platinumz inawezekana amerudiana na mama mzazi wa watoto wake Zari ambae kwa sasa yuko Afrika ya Kusini, sasa imethibitika baada ya kusambaa kwa picha ikimuonyesha msanii huyo akiwa na watoto wake.

Pamoja na kwamba mara ya kwanza alikuwa akisema amekuwa akienda kuwaona watoto wake Afrika ya kusini lakini hakukuwahi kuwa na picha iliyowahi kuthibitisha ilo mpaka jana walipotoa picha hiyo kwa mara ya kwanza kwa takribani miezi minne tangu walipokuwa wamegombana.

Picha hiyo inathibitisha kuwa kumbe wawili hao wameweka mambo yao sawa na kwa juhudi za Babu Tale kama alivyokuwa ameahidi basi yametimia. 

No comments