TALK SHOW ZIARA NILIYOIFANYA KATIKA SHULE YA SEKONDARI YA MAKONGO, KUZUNGUMZIA NGONO ZA MAPEMA NA MATUMIZI YA MITANDAO YA KIJAMII
![]() |
| Superwoman nikiongea na wanafunzi wa shule ya Makongo |
Hii
ni ziara ambayo niliamua kuifanya katika harakati za kulijengea taifa
hili vijana makini ambao tunategemea baadae kuwa viongozi
watakaoliongoza taifa hili ipasavyo.
Nilipokuwa
shule hii ya Makongo, niliweza kukutana na vijana wa vidato tofauti
tofauti na kuzungumza nao juu ya masuala mazima ya matumizi ya Mitandao
ya Kijamii 'Social Networks' mfano Facebook, Twitter, Instagram n.k;
Pamoja na suala la Ngono katika umri mdogo.
![]() |
| Wanafunzi wakisalimia kwa adabu timu nzima ya 'Wanawake Live' iliyotembelea katika shule yao ikiongozwa na Joyce Kiria |
Mitandao
ya kijamii imechukua sura tofauti hasa kwa upande wa vijana ambao
wamekuwa wakiitumia tofauti na kujikuta wakijifunza vitu visivyo na
msingi na kusahau kuwa mitandao hiyo ikitumiwa vizuri huleta maendeleo
makubwa hasa kwa upande wa elimu na maisha kiujumla.
Niliweza
kuwauliza baadhi ya wanafunzi jinsi gani wanatumia mitandao hiyo na
nilijikuta nikipata majibu tofauti huku mengine yakiwa ya msingi ingawa
sikuwa na uhakika kama ni kweli wanafunzi hao wanaitumia kama
walivyonieleza.
Suala
la ngono katika umri mdogo pia lilichukua sura yake na niliweza kusikia
maelezo tofauti kutoka kwa wanafunzi hao huku wengine wakifunguka ni
jinsi gani wameweza kukumbana na matatizo hayo na jinsi gani waliweza
kujiepusha na kutojihusisha na ngono katika umri huo mdogo.
![]() |
| Nikiteta jambo na mabinti hawa wa shule ya Makongo |
PICHA ZAIDI
![]() |
| Wanafunzi wakimsikiliza kwa makini 'The Superwoman' |
![]() |
| Nikisisitiza jambo ndani mjadala huo |
![]() |
| Vicheko vya hapa na pale ndani ya mjadala |









Post a Comment